VOOZH about

URL: https://sw.wikipedia.org/wiki/Ulaya

⇱ Ulaya - Wikipedia, kamusi elezo huru


Nenda kwa yaliyomo
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun[1]; inaitwa pia Uropa kutoka Kigiriki: "Ευρώπη", jina la mungu jike Europa) ni bara lililoko katika Kaskazini ya Dunia, likipakana na Bahari ya Aktiki upande wa kaskazini, Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi, na Bahari ya Mediterania upande wa kusini. Mpaka wake wa mashariki kwa kawaida hufafanuliwa kupitia Milima ya Ural, Mto Ural, Bahari ya Kaspi, Milima ya Kaukazi, na Bahari Nyeusi, ingawa mipaka hii ni ya kijiografia na kihistoria zaidi kuliko ya kisiasa. Kwa eneo la takriban kilomita za mraba milioni 10.18, Ulaya ni bara dogo la pili baada ya Australia lakini lina idadi kubwa ya watu, ikifikia zaidi ya milioni 750, na hivyo kuwa moja ya maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu duniani.

Ulaya ina historia ndefu na imechangia pakubwa katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, na kitamaduni duniani. Bara hili lina mataifa 44 yanayotambulika kimataifa, yakiwemo mataifa makubwa kama Ujerumani, Ufaransa, na Uingereza, pamoja na madola madogo kama Vatikani na Liechtenstein. Umoja wa Ulaya (EU) ni moja ya miungano muhimu ya kisiasa na kiuchumi katika bara hili, ukiwa na wanachama 27. Aidha, Ulaya imekuwa kitovu cha mapinduzi mbalimbali, kuanzia Mapinduzi ya Kitaaluma na ya Viwanda hadi maendeleo ya demokrasia ya kisasa, na imeendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika masuala ya kimataifa.

Ramani

👁 Image
Ulaya kutoka angani.
👁 Image
Ulaya duniani.
👁 Image
Lugha za Ulaya.
👁 Image
Kanda za kiutamaduni za Ulaya kadiri ya Ständiger Ausschuss für geographische Namen (StAGN) ya Ujerumani.
👁 Image
Ulaya mwaka 1000 hivi.

Utawala

Katika karne ya 20, baada ya vita kuu mbili, nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali:

Kanda za Ulaya

Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa (UN categorisations/map). Lakini utaratibu huo haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati. Wajerumani, Waaustria, Waswisi, Wacheki, Waslovakia na Wapolandi hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki ila Ulaya ya Kati. Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado, kwa mfano suala la Hungaria au Latvia.

Ulaya Mashariki

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
Belarus👁 Image
Minsk9,200,000
Bulgaria👁 Image
Sofia6,400,000
Jamhuri ya Czech👁 Image
Prague10,500,000
Hungary👁 Image
Budapest9,600,000
Moldova👁 Image
Chisinau2,500,000
Poland👁 Image
Warsaw37,700,000
Romania👁 Image
Bucharest19,000,000
Russia👁 Image
Moscow144,000,000
Slovakia👁 Image
Bratislava5,400,000
Ukraine👁 Image
Kyiv36,000,000

Ulaya ya Kaskazini

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
Denmark👁 Image
Copenhagen5,900,000
Estonia👁 Image
Tallinn1,300,000
Finland👁 Image
Helsinki5,600,000
Iceland👁 Image
Reykjavik380,000
Ireland👁 Image
Dublin5,100,000
Latvia👁 Image
Riga1,800,000
Lithuania👁 Image
Vilnius2,700,000
Norway👁 Image
Oslo5,500,000
Sweden👁 Image
Stockholm10,500,000
Uingereza👁 Image
London68,000,000

Ulaya ya Magharibi

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
Austria👁 Image
Vienna9,100,000
Ubelgiji👁 Image
Brussels11,800,000
Ufaransa👁 Image
Paris65,000,000
Ujerumani👁 Image
Berlin83,000,000
Liechtenstein👁 Image
Vaduz39,000
Luxembourg👁 Image
Luxembourg (jiji)660,000
Monaco👁 Image
Monaco (jiji)39,000
Uholanzi👁 Image
Amsterdam17,800,000
Uswisi👁 Image
Bern8,800,000

Ulaya ya Kusini

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
Albania👁 Image
Tirana2,800,000
Andorra👁 Image
Andorra la Vella79,000
Bosnia na Herzegovina👁 Image
Sarajevo3,200,000
Kroatia👁 Image
Zagreb3,800,000
Cyprus👁 Image
Nicosia1,200,000
Ugiriki👁 Image
Athens10,200,000
Italia👁 Image
Rome59,000,000
Malta👁 Image
Valletta520,000
Montenegro👁 Image
Podgorica620,000
Macedonia Kaskazini👁 Image
Skopje1,800,000
San Marino👁 Image
San Marino (mji)34,000
Serbia👁 Image
Belgrade6,600,000
Slovenia👁 Image
Ljubljana2,100,000
Hispania👁 Image
Madrid47,800,000
Vatican City👁 Image
Vatican City (mji)800
Ureno👁 Image
Lisbon10,100,000

Nchi za Ulaya

Orodha kamili ya nchi za Ulaya ikitaja ukubwa wa eneo, idadi ya watu, miji mikuu na miji mikubwa zaidi pamoja na lugha rasmi. Orodha hii haionyeshi ukanda wa nchi husika. Tazama juu kupata kanda za Ulaya.

Orodha ya Nchi na Maeneo ya Ulaya
BenderaNchi/MaeneoEneo (km²)Idadi ya WatuMji MkuuJiji KubwaLugha Rasmi
👁 Image
Albania28,7482,829,741TiranaTiranaKialbania
👁 Image
Andorra46879,034Andorra la VellaAndorra la VellaKihispania
👁 Image
Armenia29,7432,767,923YerevanYerevanKiarmenia
👁 Image
Austria83,8799,006,398ViennaViennaKijerumani
👁 Image
Azebajani (zaidi ni Asia)86,60010,353,269BakuBakuKiazabajani
👁 Image
Aislandi103,000366,425ReykjavikReykjavikKiaislandi
👁 Image
Ayalandi70,2734,994,724DublinDublinKiingereza, Kigaeli
👁 Image
Belarusi207,6009,349,645MinskMinskKibelarusi, Kirusi
👁 Image
Bulgaria110,9936,447,710SofiaSofiaKibulgaria
👁 Image
Bosnia na Herzegovina51,1973,276,000SarajevoSarajevoKiserbia, Kikroeshia, Kibosnia
👁 Image
Estonia45,2271,331,796TallinnTallinnKiestonia
👁 Image
Hungaria93,0289,606,259BudapestBudapestKihungaria
👁 Image
Italia301,34060,317,116RomeRomeKiitalia
👁 Image
Jojia (zaidi ni Asia)69,7003,688,600TbilisiTbilisiKijojia
👁 Image
Korasia56,5943,850,695ZagrebZagrebKikorasia
👁 Image
Kosovo10,8871,798,188PristinaPristinaKikosovo
👁 Image
Kupro9,2511,244,188NicosiaNicosiaKigiriki, Kituruki
👁 Image
Latvia64,5891,882,000RigaRigaKilatvia
👁 Image
Liechtenstein16039,315VaduzSchaanKijerumani
👁 Image
Lithuania65,3002,794,000VilniusVilniusKilithuania
👁 Image
Luxembourg2,586634,814Luxembourg CityLuxembourg CityKifaransa, Kijerumani, Kiluxembourg
👁 Image
Malta316514,564VallettaBirkirkaraKimalta, Kiingereza
👁 Image
Moldova33,8462,603,000ChisinauChisinauKimoldova
👁 Image
Monako2.0239,511MonacoMonacoKifaransa
👁 Image
Norwei385,2075,391,369OsloOsloKinorwei
👁 Image
Polandi312,69638,265,017WarsawWarsawKipolandi
👁 Image
San Marino6133,600San MarinoSan MarinoKiitalia
👁 Image
Ubelgiji30,68911,584,008BrusselsAntwerpKiholanzi, Kifaransa, Kijerumani
👁 Image
Ucheki78,86610,686,269PraguePragueKicheki
👁 Image
Udeni42,9255,932,654CopenhagenCopenhagenKideni
👁 Image
Ufaransa551,69568,042,591ParisParisKifaransa
👁 Image
Ufini338,4245,541,037HelsinkiHelsinkiKifini, Kiswidi
👁 Image
Ufalme wa Muungano243,61067,736,802LondonLondonKiingereza
👁 Image
Ugiriki131,95710,724,599AthensAthensKigiriki
👁 Image
Uhispania505,99047,450,795MadridMadridKihispania
👁 Image
Uholanzi41,54317,407,585AmsterdamRotterdamKiholanzi
👁 Image
Ujerumani357,02283,190,556BerlinBerlinKijerumani
👁 Image
Ureno92,09010,295,909LisbonLisbonKireno
👁 Image
Urusi (Sehemu ya Ulaya)17,098,242146,599,183MoscowMoscowKirusi
👁 Image
Vatikani0.49825Vatican CityVatican CityKilatini, Kiitalia

Tanbihi

1. Kanda zinazotajwa (Ulaya ya Kusini – magharibi n.k.) zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisations/map. Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine (Asia, Afrika, au Oceania). Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti; pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao.

2. Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia; namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee.

3–5. Guernsey, Kisiwa cha Man, and Jersey ni maeneo ya kujitegemea chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza.

6. Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira, ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika.

7. Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika, wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani ya Moroko, Afrika ya Kaskazini.

8. Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini, Bahari Hindi au Oceania.

9. Uholanzi: Idadi ya wakazi ni ya 2004; Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali.

10. Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki

11. Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

12. Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus.

13. Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

14. Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul.

15. Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

Tazama pia

Marejeo

  1. Hivyo asili ya neno "Ulaya" ni sawa na "wilaya"; Krapf 1882 Swahili-English dictionary anaeleza: ""ULAYA (WALAYA au WILAYA ya) ... mother-country in contradistinction to colonies, foreign possessions or parts"; Sacleux 1939 Dictionnaire Swahili-Francais anataja kama etimolojia ya Ulaya "Ar. Hind. ولاية wilaya, pays etranger" (=nchi ya kigeni); Madan 1903 "Wilaya, n. (1) native land, home, but commonly used of foreigners, and so (2) Europe. Ulaya Uzungu, Europe. U, Hindi, India. Ulaya wa Wareno, Portugal