VOOZH about

URL: https://www.trtafrika.com/swahili/article/7633920cd541

⇱ Bado bao moja tu kwa Lionel Messi kuweka historia - TRT Afrika


| Swahili
| Swahili
MICHEZO
1 dk kusoma
Bado bao moja tu kwa Lionel Messi kuweka historia
Messi ameweka rekodi mpya kwa kuwa mchezaji wa kwanza kushiriki Kombe la Dunia mara sita.
πŸ‘ Bado bao moja tu kwa Lionel Messi kuweka historia
Messi amecheza mechi yake ya 200 katika timu ya taifa ya Argentina. / / Reuters

Lionel Messi alianza kampeni yake ya sita ya Kombe la Dunia kwa kishindo baada ya kufunga ''hat-trick''. Mafanikio hayo yaliisaidia Argentina, mabingwa watetezi, kuanza harakati za kutetea taji lao kwa ushindi mkubwa wa magoli 3-0 dhidi ya Algeria katika mechi ya Kundi J.

Messi mwenye umri wa miaka 38 aliifanya siku hiyo kuwa ya kihistoria kwa kucheza mechi yake ya 200 katika timu ya taifa.

ZILIZOPENDEKEZWA
ZILIZOPENDEKEZWA

Pia aliweka rekodi mpya kwa kuwa mchezaji wa kwanza kushiriki Kombe la Dunia mara sita, katika mechi yao dhidi ya Algeria.

Kwa magoli hayo matatu, Messi alifikisha jumla ya 16 katika historia ya Kombe la Dunia na kuwa sawa na rekodi iliyowekwa na mchezaji wa Ujerumani, Miroslav Klose, kama wafungaji bora wa mashindano hayo.

CHANZO:TRT Afrika
ZILIZOPENDEKEZWA
ZILIZOPENDEKEZWA
Soma zaidi